Wednesday, July 24, 2013

Kocha amtema Mnigeria Ogbu Chukwadi
Ogbu Chukwadi
WAKATI Kocha Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts, amemuondoa kwenye programu zake mshambuliaji wa kimataifa raia wa Nigeria, Ogbu Chukwadi, timu hiyo inatarajiwa kuweka kambi nje ya nchi.
Chanzo cha habari kutoka ndani ya klabu hiyo kiliipasha chanzo chetu cha habari kwa sharti la kutotajwa jina kuwa Brandts ameufikishia maoni uongozi wake kuwa hahitaji kufanya kazi na mshambuliaji huyo ambaye alifanikiwa kumuona siku moja na kuumia hadi sasa.
Aidha, chanzo hicho kilisema kuwa wakati akiwasilisha mapendekezo ya kumtema Ogbu, yaliambatana na mahali pa kuweka kambi kwa ajili ya Ngao ya Jamii, Ligi Kuu na michuano ya kimataifa.
“Kocha yeye ndiye hamtaki katika programu zake Ogbu na tayari ameuambia uongozi, maana anaonekana kutokuwa na umuhimu katika timu yetu japokuwa anarekodi nzuri kisoka,” alisema mtoa habari huyo.
Aliongeza kuwa kutokana na kumkosa mchezaji huyo, kocha ameutaka uongozi kuhakikisha wanamtafutia walau washambuliaji wawili, kwa kuwa kuna upungufu katika safu ya ushambuliaji ambao unahitaji maboresho.
Alisema mapendekezo makubwa ya kocha ni kurudi nchini Uturuki ambako kuna hali ya hewa nzuri iliyowafanya kutwaa ubingwa msimu uliopita na kuwa endapo uongozi utashindwa katika nchi hiyo, usake nyingine yenye hali ya hewa kama hiyo.
Licha ya Brandts kumtema kikosini mwake mchezaji huyo, siku anawasili, Katibu Mkuu wa klabu hiyo, Lawrence Mwalusako, alisema kuwa huyo si mchezaji bali ni mfanyabiashara mwenzake.
Kazimoto arejea kimiujiza
HATIMAYE kiungo wa Simba, Mwinyi Kazimoto, aliyetimkia nchini Qatar amerejea jijini Dar es Salaam kimya kimya huku uongozi wa klabu yake ukiwa haufahamu kuhusu ujio wake.
Kazimoto alitoweka bila taarifa akiwa timu ya taifa ‘Taifa Stars’ baada ya kumalizika kwa mchezo wa awali dhidi ya Uganda, uliomalizika kwa Stars kulala bao 1-0 na nafasi yake kuwa matatani.
Kutokana na kitendo chake hicho, nafasi yake timu ya taifa ilizibwa na Mudathir Yahya wa Azam FC.
Habari ilizozipata Tanzania Daima jana kutoka kwa mtu wa karibu na Kazimoto, zilisema kuwa alionekana eneo la Kinondoni Moscow usiku wa juzi akiwa na baadhi ya wachezaji wa moja ya timu za Ligi Kuu Tanzania Bara inayomilikiwa na moja ya majeshi ya hapa nchini.
“Mnahangaika kumtafuta na kujiuliza Kazimoto yuko wapi, mimi nimemuona jana Kinondoni kwa macho yangu akiwa na wachezaji wa ... ila alikuwa kweli nje ya nchi na amerudi,” alisema mtoa habari huyo.
Aidha, chanzo hicho kilienda mbali na kubainisha kuwa kiungo huyo ameshindwa kufuzu alikokuwa ndiyo sababu ya kurejea kimya kimya bila ya kuutaarifu uongozi.
Baada ya kurejea, Kazimoto anatarajiwa kukumbana na adhabu kutoka Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kutokana na utovu wa nidhamu aliouonesha, huku pia klabu yake nayo ikitarajiwa kumpa adhabu pia.
Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah, alikaririwa hivi karibuni kuwa, Kiungo huyo endapo atapatikana atapewa adhabu kutokana na kanuni ambazo alisaini wakati akiingia kambini zinavyosema.
Kwa upande wa Simba, Katibu wake Mkuu, Evodius Mtawala, alikiri kusikia taarifa hizo na kudai kuwa wanamsubiri arejee kundini, kwa kuwa ana mkataba na klabu hiyo.
“Tumesikia tu, ila bado hatujamuona, tunamsubiri akija mwenyewe klabuni ndipo tutajua jinsi ya kumwadhibu, kwani aliondoka bila ya kututaarifu,” alisema Mtawala.
Higuain apasi vipimo Napoli
Gonzalo Higuain chini ya ulinzi mkali
MSHAMBULIAJI wa Gonzalo Higuain wa Real Madrid ametanguliza mguu mmoja Napoli ya Italia baada ya kupasi vipimo vya afya na kwa hivyo Napoli imesema itamtambulisha rasmi siku ya J,tatu usiku.
 Napoli imekubali kulipa kitita cha euro mil 42.3 kama gharama ya uamisho wake kutoka Madrid
Mbali ya dau hilo, nyota huyo raia wa Argentina atakayekuwa chini ya Kocha Rafael Benitez, atakuwa akilipwa mshahara wa euro 163,000 kwa wiki chini
Awali, Napoli walishatoa ofa ya euro milioni 37, lakini sasa imefikia kiwango hicho kutokana na gharama nyinginezo za mchezaji binafsi.
Baada ya majadiliano ya kina baina ya pande zote, jambo hilo limefika mwisho ambapo nyota huyo atang’oka Santiago Bernabeu kwa kitita hicho cha euro mil 42.3
Higuain anangoka licha ya kocha mpya wa Real Madrid, Carlo Ancelotti hivi karibuni kusema kuwa mchezaji huyo asingeondoka, lakini jana alimwacha nyota huyo katika mechi ya kirafiki dhidi ya Lyon.
Jeuri ya Napoli katika usajili, inatokana na mauzo
ya Edinson Cavani aliyetua Paris Saint-Germain kwa kitita cha euro mil 63.
Kwa nyota huyo kwenda Napoli, kumefuta juhudi za Arsenal kumwania nyota huyo ambayo baada ya kuona ugumu, iliahirisha jambo hilo hadi Juni.
Suarez ataka kuteta na Arsenal
JUHUDI za Arsenal kumwania mshambuli wa kimataifa wa Uruguay anayechezea Liverpool ya England, Luis Suarez huenda sasa zikaanza kuzaa matunda baada ya nyota huyo kuataka kufanya nao mazungumzo.
Suarez atakayekosa mechi za mwanzoni mwa msimu wa Ligi Kuu, anaamini dau la pauni mil 40 la Arsenal, linakidhi matakwa ya mkataba wake.
Suarez anasema kuna uwezekano Liverpool ilitafsiri vibaya kipengele katika mkataba, hivyo amepanga kumweleza kocha wake
Brendan Rodgers anataka kukutana na Arsenal.
Kauli ya nyota huyo mtukutu, kunahuisha harakati za Arsenal kumwania mchezaji huyo licha ya ofa zake mbili kutupwa.
Hata hivyo, baada ya Arsenal kushindwa kumpata Gonzalo Higuain wa Real Madrid ambaye ametimikia Napoli, nguvu zote sasa imeelekeza kwa Suarez.
Suarez ni miongoni mwa wachezaji wa kutumainiwa katika kikolsi cha Liverpool, akiifungia mabao 30 katika mechi 44.
Tangu ajiunge na Liverpool Januari, 2011 akitokea Ajax  ya Uholanzi kwa kitita cha pauni mil 22.7, ameifungia jumla ya mabao m, 51 katika mechi 96.
Kabla ya Liverpool, Suarez aliondoka Ajax baada ya kuifungia mabao 49 katika mechi 48 huku akiifungia Uruguay mabao 31 katika mechi 62.
Wakati hayo yakiendelea, uwezekano wa Arsenal kumtwaa Suarez ni mkubwa baada ya kufikia dau la pauni mil 40 ambalo linaendana na kipengere cha mkataba.
Liverpool ikikuna kichwa kumbakisha nyota huyo, uwezekano wa kuondoka ni mkubwa kama Arsena itapanda zaidi ya dau hilo.
Kauli hiyo chungu ya Suarez inakuja siku chache tu tangu kocha wa Liverpool ashushe pumzi baada ya nyota huyo kujiunga na timu ziarani Asia na Australia.
Aliungana na wenzake tangu Jumapili iliyopita mjini  Melbourne, akitokea kwenye mapumziko baada ya michuano ya Kombe la Mabara nchini Brazil.
Garvinho ang’oka Arsenal
KLABU ya AS Roma ya Italia imekaribia kumtwaa nyota wa kimataifa
wa Ivory Coast, Garvinho kwa kitita cha pauni mil 8 akitokea Arsenal ya England.
Hiyo ni kutokana na juhudi za AS Roma waliofunga safari hadi Emirates kuzungumza na viongozi wa Arsenal kwa siku ya juzi na jana na leo huku kukiwa na uwezekano mkubwa wa pande hizo kufikia muafaka.
Kimsingi pande  hizo mbili zimeshafikia muafaka kuhusu dau, kilichokuwa bado kinadiliwa ni mengine yanayohusu mkataba ikiwemo mshahara kwani Roma wanataka wamlipe  pauni 50,000 kwa wiki kama wa Arsenal.
Hesabu za Arsenal ni kumuuza Gervinho kutoa nafasi ya ujio wa Luis Suarez na Marouane Fellaini japo bado inawaota Cesc Fabregas na Wayne Rooney.
Ndio maana Gervinho ameachwa katika ziara ya maandalizi ya msimu ujao barani Asai kwa maelezo
kuwa nyota huyo yu mgonjwa
Presha ya Roma kumtaka Garvinho inachagizwa na
kocha Rudi Garcia, aliyewahi kumnoa nyota huyo kwa msimu mwili akiwa na Lille ya Ufaransa kabla ya kutua
Arsenal mwaka 2011.
Micho Taifa Stars inaniumiza kichwa
Awakosa Tony Odur na Patrick Edema


WAKATI msfara wa timu ya soka ya Tanzania Taifa Stars ukitarajiwa kutua mjini Kampala, Uganda tangu jana mchana, Kocha wa Uganda Cranes, Sredojevic Milutin Micho, amesema katika mechi hiyo ya Jumamosi vijana wake watashambulia kwa dakika zote.
Micho ambaye kikosi chake kimeingia kambini juzi kutokana na yeye kuwa safarini nchini Ethiopia kufuatilia viwango vya nyota wake watatu wanaochezea St. George ambayo mwishoni mwa wiki ilicheza mechi ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Stade de Malien ya Mali.
Nyota waliompeleka Micho Ethiopia, ni Robert Ssentongo, Robert Odongkara na Isaac Isinde na kuwashuhudia vijana wake wakiisaidia St. George kushinda mabao 2-0 katika mechi ya kwanza ya hatua ya makundi.
"Tutawakabili Stars kwa kuanza kufunga kuanzia mwanzoni mwa mchezo. Kwa bahati mbaya, hatuna muda.
“Ninachotaka kufanya sasa ni kuwasaidia wachezaji kujielekeza kwenye mechi. Nitakachofanya ni kuwafundisha kucheza kwenye nafasi na kufanya kile kisichotarajiwa, kufungua nafasi na kuwadhibiti wapinzani,” alisema Micho.
Cranes itaikabili Stars ikiwa na tatizo la ufungaji kwani katika mechi mbili za kirafiki ilizocheza na vijana wa chini ya miaka 23 (U-23 Kobs) na kufungwa zote kwa  bao 1-0 ambapo Denis Iguma alicheza sehemu ya kiungo.
Mbali ya ubutu wa safu ya ushambuliaji, pia Micho atawakosa wachezaji wake wawili wa mbele,
Tony Odur na Patrick Edema. Wakati Odur anauguza nyonga, Edema amekwenda Ureno kwa majaribio.
Micho amewaita nyota wengine Simon Okwi (KCC FC), David Kasirye (URA FC) na Henry Oguti anayechezea Kiira Young.
Hata hivyo, Okwi ameitwa licha ya kushindwa kufungia bao KCC msimu uliopita huku kukiwa na shaka juu ya kiwango cha Kasirye.
Mazingira hayo yanamfanya Micho amtegemee Oguti kuongoza safu ya ushambuliaji anayeonekana kuwa na nguvu kuliko wengine ingawa kuna mwingine kama Frank Kalanda.
Mshambuliaji wa Taifa Stars, John Boko akijaribu kuumiliki mpira