Wednesday, July 24, 2013

Micho Taifa Stars inaniumiza kichwa
Awakosa Tony Odur na Patrick Edema


WAKATI msfara wa timu ya soka ya Tanzania Taifa Stars ukitarajiwa kutua mjini Kampala, Uganda tangu jana mchana, Kocha wa Uganda Cranes, Sredojevic Milutin Micho, amesema katika mechi hiyo ya Jumamosi vijana wake watashambulia kwa dakika zote.
Micho ambaye kikosi chake kimeingia kambini juzi kutokana na yeye kuwa safarini nchini Ethiopia kufuatilia viwango vya nyota wake watatu wanaochezea St. George ambayo mwishoni mwa wiki ilicheza mechi ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Stade de Malien ya Mali.
Nyota waliompeleka Micho Ethiopia, ni Robert Ssentongo, Robert Odongkara na Isaac Isinde na kuwashuhudia vijana wake wakiisaidia St. George kushinda mabao 2-0 katika mechi ya kwanza ya hatua ya makundi.
"Tutawakabili Stars kwa kuanza kufunga kuanzia mwanzoni mwa mchezo. Kwa bahati mbaya, hatuna muda.
“Ninachotaka kufanya sasa ni kuwasaidia wachezaji kujielekeza kwenye mechi. Nitakachofanya ni kuwafundisha kucheza kwenye nafasi na kufanya kile kisichotarajiwa, kufungua nafasi na kuwadhibiti wapinzani,” alisema Micho.
Cranes itaikabili Stars ikiwa na tatizo la ufungaji kwani katika mechi mbili za kirafiki ilizocheza na vijana wa chini ya miaka 23 (U-23 Kobs) na kufungwa zote kwa  bao 1-0 ambapo Denis Iguma alicheza sehemu ya kiungo.
Mbali ya ubutu wa safu ya ushambuliaji, pia Micho atawakosa wachezaji wake wawili wa mbele,
Tony Odur na Patrick Edema. Wakati Odur anauguza nyonga, Edema amekwenda Ureno kwa majaribio.
Micho amewaita nyota wengine Simon Okwi (KCC FC), David Kasirye (URA FC) na Henry Oguti anayechezea Kiira Young.
Hata hivyo, Okwi ameitwa licha ya kushindwa kufungia bao KCC msimu uliopita huku kukiwa na shaka juu ya kiwango cha Kasirye.
Mazingira hayo yanamfanya Micho amtegemee Oguti kuongoza safu ya ushambuliaji anayeonekana kuwa na nguvu kuliko wengine ingawa kuna mwingine kama Frank Kalanda.
Mshambuliaji wa Taifa Stars, John Boko akijaribu kuumiliki mpira

No comments:

Post a Comment