Wednesday, July 24, 2013

Suarez ataka kuteta na Arsenal
JUHUDI za Arsenal kumwania mshambuli wa kimataifa wa Uruguay anayechezea Liverpool ya England, Luis Suarez huenda sasa zikaanza kuzaa matunda baada ya nyota huyo kuataka kufanya nao mazungumzo.
Suarez atakayekosa mechi za mwanzoni mwa msimu wa Ligi Kuu, anaamini dau la pauni mil 40 la Arsenal, linakidhi matakwa ya mkataba wake.
Suarez anasema kuna uwezekano Liverpool ilitafsiri vibaya kipengele katika mkataba, hivyo amepanga kumweleza kocha wake
Brendan Rodgers anataka kukutana na Arsenal.
Kauli ya nyota huyo mtukutu, kunahuisha harakati za Arsenal kumwania mchezaji huyo licha ya ofa zake mbili kutupwa.
Hata hivyo, baada ya Arsenal kushindwa kumpata Gonzalo Higuain wa Real Madrid ambaye ametimikia Napoli, nguvu zote sasa imeelekeza kwa Suarez.
Suarez ni miongoni mwa wachezaji wa kutumainiwa katika kikolsi cha Liverpool, akiifungia mabao 30 katika mechi 44.
Tangu ajiunge na Liverpool Januari, 2011 akitokea Ajax  ya Uholanzi kwa kitita cha pauni mil 22.7, ameifungia jumla ya mabao m, 51 katika mechi 96.
Kabla ya Liverpool, Suarez aliondoka Ajax baada ya kuifungia mabao 49 katika mechi 48 huku akiifungia Uruguay mabao 31 katika mechi 62.
Wakati hayo yakiendelea, uwezekano wa Arsenal kumtwaa Suarez ni mkubwa baada ya kufikia dau la pauni mil 40 ambalo linaendana na kipengere cha mkataba.
Liverpool ikikuna kichwa kumbakisha nyota huyo, uwezekano wa kuondoka ni mkubwa kama Arsena itapanda zaidi ya dau hilo.
Kauli hiyo chungu ya Suarez inakuja siku chache tu tangu kocha wa Liverpool ashushe pumzi baada ya nyota huyo kujiunga na timu ziarani Asia na Australia.
Aliungana na wenzake tangu Jumapili iliyopita mjini  Melbourne, akitokea kwenye mapumziko baada ya michuano ya Kombe la Mabara nchini Brazil.

No comments:

Post a Comment