Tuesday, July 23, 2013

Kivuli cha Ferguson chamtesa Moyes
KOCHA David Moyes aliyeziba nafasi ya Sir Alex Ferguson tangu miezi miwili iliyopita baada ya kuinoa timu hiyo kwa miaka 27, anakabiliwa na kibarua kigumu cha kujenga heshima yake ndani ya Old Trafford.
Kibarua kwake ni kuyalinda kwa kuyaendeleza mafanikio makubwa ya timu hiyo yaliyopatikana chini ya Ferguson (71) ambaye ameondoka baada ya kuipa mataji lukuki yakiwamo 13 ya Ligi Kuu, mawili ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, Klabu Bingwa ya Dunia na mengine ya ndani. 
Ferguson kwa upande wake anaamini Moyes ni mtu sahihi atakayeweza kulinda heshima ya klabu hiyo na kuwataka wapenzi kumpa sapoti katika jukumu hilo akitokea Everton alikodumu kwa miaka 11.
Moyes yeye anajiamini kuwa ni mtu sahihi wa kuziba nafasi hiyo akisema hizi ni zama zake, hivyo ni jukumu lake kuiwezesha timu hiyo kuanza kuandika historia mpya chini yake.
"Hizi ni zama zangu," alisema. Nimechukua nafasi na nipo kazini. Ni wakati wangu wa kuweka historia.
"Tangu siku ya kwanza nilipokuja hapa, nilisema nitamtumia Ferguson kwa vile ni mtu menye maarifa mengi.
"Lakini, ukweli ni kuwa bado jukumu hili sasa ni langu, ninapaswa kulibeba. Unapofikiria mafanikio ya Sir. Matt Busby na Sir Alex Ferguson katika historia ya klabu hii, nina kazi kubwa ya kufanya.
"Ni jukumu langu sasa kuhakikisha nami ninajenga historia yangu katika klabu hii kwani hicho ndocho kinasubiriwa kwa hamu na wapenzi wa klabu hii kote duniani.
"Siweze tena kumtegemea Sir Alex kwa kila jambo, ingawa nitabaki kuyaheshimu mafanikio yake (Ferguson).  
"Nitabaki kumheshimu Ferguson kama Manchester United ambavyo wamekuwa wakifanya mara zote."
Hata hivyo, Moyes amekiri kuwa angependa kupata mafanikio kama ya hao watangulizi wake japo anajimini katika kazi yake kwamba ni mtu sahihi katika nafasi hiyo ndani ya Manchester United.
Kipimo cha awali kwa Moyes, ni kutetea ubingwa wa Ligi Kuu itakayoanza Agosti 17 kwa kuwafuata Swansea City kabla ya kuzivaa Chelsea, Liverpool, Crystal Palace na jirani zao Manchester City.
Kwa upande mwengine Man United leo imepewa kichapo cha goli 3-2 kutoka kwa Yokohama F Marinos ya Japan.Katika mechi hiyo mabao ya Yokohama F Marinos yametiwa kambani na M MARQUINHOS, F AGUIAR,Y FUJITA, huku United wakijipatia mabao yao kutoka kwa LINDARD na lengine TASHIRO ambaye ni mchezaji wa Yokohama aliyejifunga.
Shinji Kagawa (kulia) akiwa kwenye hekaheka uwanjani.

No comments:

Post a Comment