Tuesday, July 23, 2013

Simba yamnyatia Owino
TIMU ya Simba imeanza mkakati wa kumrejesha beki wake wa zamani, George Owino anayekipiga URA ya Uganda ambayo ilikuwa nchini kwa mechi mbili za kirafiki dhidi ya timu za Simba na Yanga.
Jumamosi iliyopita, URA waliifunga Simba mabao 2-0 katika Uwanja wa Taifa, jijiji Dar es Salaam kabla ya kutoka sare ya 2-2 dhidi ya Yanga siku iliyofuata huku Owino akimudu vema safu ya ulinzi hadi kuwavutia Msimbazi kutakani kumrejesha.
Baada ya filimbi ya mwisho, Meneja wa Simba na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Zacharia Hans Pope, waliteta  na beki huyo wakitaka arejee Msimbazi huku kukiwa na habari kuwa jana alitarajiwa kusaini fomu kama dau lake la dola 35,000 za Marekani litaafikiwa.
Owino anatua Msimbazi ikiwa ni siku chache tangu nyota wanne wa kimataifa waliokuwa wakisaka namba katika timu hiyo chini ya Kocha Abdallah Kibadeni kuwachuja wanne waliokuwa wakipigania kusajiliwa kutokana na kutoridhishwa na viwango vyao.  
“Nashukuru viongozi wananihitaji baada ya kuvutiwa na kiwango changu…sina wasiwasi kabisa kama wakifikia fedha ninayotaka nitarudi Simba kwani ni timu ninayoipenda,” alisema Owino
Habari ambazo zilipatikana jana kutoka ndani ya klabu hiyo zilizisema nyota huyo pande hizo mbili zimeendelea kuzungumza kwani kiasi anachotaka ni kikubwa kulingana na uwezo wa Simba, wakitaka kumpatia dola 25,000.
“Kuna mvutano kidogo katika majadiliano yetu, lakini naamini watafikia muafaka kwani uongozi na Kocha Kibadeni wamemkubali,” kiliongeza chanzo hicho.
Simba pia imeachana na nyota wanne wa kigeni waliokuwa wakisaka namba huku ikisitisha mkataba wa miaka miwili na kiungo wake Mganda, Mussa Mudde kwa kutodhishwa na kiwango.
Katibu Mkuu wa klabu hiyo, Evodius Mtawala alisema wameachana na nyota hao wanne waliokuwa wakisaka namba na Mude, isipokuwa kipa Abel Dhaira na Amissi Tambwe kutoka Burundi.
Aliwataja walioachwa ni Assumani Buyinza na Samuel Ssenkoomi (Uganda) na Felix Cuipo (DR Congo) na James Kun, raia wa Sudan Kusini ambao wameshindwa kumridhisha Kibadeni.
Mtawala alisema nyota hao wameshapewa na tiketi za kurudi makwao huku  uongozi ukiwa umemalizana na Mudde ambaye alikuwa na mkataba wa miaka miwili.

No comments:

Post a Comment