Wednesday, July 24, 2013

Garvinho ang’oka Arsenal
KLABU ya AS Roma ya Italia imekaribia kumtwaa nyota wa kimataifa
wa Ivory Coast, Garvinho kwa kitita cha pauni mil 8 akitokea Arsenal ya England.
Hiyo ni kutokana na juhudi za AS Roma waliofunga safari hadi Emirates kuzungumza na viongozi wa Arsenal kwa siku ya juzi na jana na leo huku kukiwa na uwezekano mkubwa wa pande hizo kufikia muafaka.
Kimsingi pande  hizo mbili zimeshafikia muafaka kuhusu dau, kilichokuwa bado kinadiliwa ni mengine yanayohusu mkataba ikiwemo mshahara kwani Roma wanataka wamlipe  pauni 50,000 kwa wiki kama wa Arsenal.
Hesabu za Arsenal ni kumuuza Gervinho kutoa nafasi ya ujio wa Luis Suarez na Marouane Fellaini japo bado inawaota Cesc Fabregas na Wayne Rooney.
Ndio maana Gervinho ameachwa katika ziara ya maandalizi ya msimu ujao barani Asai kwa maelezo
kuwa nyota huyo yu mgonjwa
Presha ya Roma kumtaka Garvinho inachagizwa na
kocha Rudi Garcia, aliyewahi kumnoa nyota huyo kwa msimu mwili akiwa na Lille ya Ufaransa kabla ya kutua
Arsenal mwaka 2011.

No comments:

Post a Comment