Saturday, July 27, 2013

Demba Ba namuogopa Rooney Chelsea
MSHAMBULIAJI, Demba Ba, amekana taarifa kuwa anajiandaa kutimka klabuni Stamford Bridge, kukimbia ujio wa Wayne Rooney kama Chelsea itafanikiwa kupata saini ya nyota huyo wa kimataifa wa England.
Badala yake, Ba nyota wa kimataifa wa Senegal amemkaribisha kwa mikono miwili, Rooney anayechezea Manchester United, huku akiongeza kuwa Darajani ni sehemu sahihi ya ushindani na yu tayari kwa vita ya namba.
Ba ameongeza kuwa anawakaribisha wakali zaidi wa safu ya mbele klabuni hapo, ili kuwaongezea nguvu yeye, Fernando Torres na Romelu Lukaku.
“Nadhani tunahitaji ushindani na tunawakaribisha washambuliaji na wachezaji bora katika kikosi chetu. Ushindani kikosini utanifanya mimi kuwa bora dimbani kwa kila namna.
“Bila shaka wachezaji wote wanataka kucheza, si tu washambuliaji wa kati. Lakini tutafanya kazi kwa pamoja kama timu katika huo huo, kwa manufaa na ustawi wa klabu, kujaribu na kushinda michezo. Hivyo basi, ndiyo nitabaki hapa hata akija Rooney.”
Ba alifunga moja ya mabao ya Chelsea katika ushindi wa mabao 8-1 dhidi ya Indonesia XI juzi usiku mbele ya mashabiki wapatao 65,000 na amekiri kuwa itakuwa na msisimko wa aina yake kwake kucheza msimu huu chini ya kocha mpya Jose Mourinho.
Aliongeza kuwa: “Daima inakuwa ni jambo zuri mno kufunga, lakini katika hatua hii zaidi inakuwa ni kuhusu kuwajibika na kukaza msuli ipasavyo dimbani ili kurejea hali uhatari kama ilivyokuwa huko nyuma.
“Najisikia vizuri. Imekuwa wiki nzuri kikazi chini ya kocha mpya. Tutaona mambo yatakuwaje katika wiki chache zijazo. Itakuwa hali ya kusisimua sana,” alitamba Ba

No comments:

Post a Comment