Monday, July 22, 2013

Arsenal yaendelea kutoa dozi Asia
Wachezaji wa Arsenal wakishangilia goli
Timu ya Arsenal inaendelea na wimbi la ushindi mnono katika ziara ya kujiandaa kwa msimu mpya wa Ligi Kuu England, kwa mara nyingine tena imeipiga Nagoya Grampus Eight ya Japan kwa jumla ya mabao 3-1.
Mabao hayo yakitiwa kambani na Olivier Giroud, Walcott na mjapani wao anaikipiga Arsenal Ryo Miyaichi.
Kwa ushindi huo wapiga bunduki hao wa London wamefikisha jumla ya ponti 9 na mabao 17. Je, kwa kasi hiyo wataendelea nayo mpaka kwenye ligi au ndiyo nguvu ya soda?
Ligi Kuu ya Vodacom 2013/2014 
Kuanza kutimua vumbi Agosti 24
Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) 2013/2014 inaanza kutimua vumbi Agosti 24 mwaka huu kwa timu zote 14 katika miji saba tofauti hapa nchini.
Hata hivyo, kabla ya ligi hiyo kuanza kutakuwa na mechi ya kufungua msimu (Ngao ya Jamii- Community Shield) kati ya bingwa mtetezi Yanga na Timu iliyoshika nafasi ya pili ya msimamo naizungumzia Azam itakayochezwa Agosti 17 ndani ya dimba la Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Mechi za VPL za Agosti 14 mwaka huu zitakuwa kama ratiba inavyoonesha hapo chini:-