Monday, September 2, 2013

Kaka arejea nyumbani AC Milan

Kaka arejea nyumbani AC Milan
MAKAMU wa rais wa klabu ya AC Milan, Adriano Galliani amethibitisha klabu yake kumsainisha mchezaji Ricardo Kaka anayekipiga Real Madrid.
Kaka anatarajiwa kurejea Milan, ambako anaamini atafurahia maisha yake ya soka, baada ya kukaa Bernabeu kwa muda wa miaka minne kwa dili la pauni milioni 56.
Mchezaji huyo mwenye miaka 31 amekubali kusaini mkataba wa miaka miwili mwishoni mwa wiki hii.
Kaka alikosa raha katika muda wake wa uchezaji kutokana na kusombuliwa na majeruhi.
Lakini mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazil anaamini kiwango chake kitarudi kama zamani mara ya kwanza alipokuwa San Siro.
Taarifa za Milan zimeeleza kuwa: "usiku wa jana tumeboresha zaidi uhusiano wetu na klabu za Real Madrid kwa kuwezesha kuturudishia mchezaji Ricardo Kaka.

No comments:

Post a Comment