Thursday, August 29, 2013

Yanga SC yashikwa, Mnyama aua

Yanga SC yashikwa, Mnyama aua
Abdi Banda kati kati akiwatoka wachezaji wa Yanga.
 Jerry Santo akipiga penati iliyozaa goli dakika ya 90.
MABINGWA watetezi wa Lgi Kuu Tanzania Bara, Yanga SC jana walilazimishwa sare ya bao 1-1 na Coastal Union ya Tanga katika mechi iliyochezwa Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Yanga walipata bao dakika ya 68, na Mshambuliaji wao hatari Didier Kavumbagu baada ya kupokea krosi safi iliyopigwa na David Luhende.
Hivyo, Coastal Union walisawazisha dakika ya 90 kwa mkwaju wa penalti iliyofungwa na Jerry Santo, baada ya Luhende kuunawa mpira ndani ya kumi na nane.
Hivyo kila timu ikanyakua pointi moja, na kufikisha pointi nne kila mmoja katika.
Baada ya mechi kumalizika, polisi waliamua kuwatawanya mashabiki wa Yanga kwa kutumia mabomu ya machozi, kutokana na kufanya fujo kwa kukerwa na uchezeshaji wa mwamuzi.
Wale watani wao wa Jadi, Simba ilipata ushindi mwembamba wa bao 1-0 kutoka kwa JKT Oljoro.
Nayo Ashanti United jana imeendelea kuwa mdebwedo baada ya kuchapwa bao 1-0 na JKT Mgambo.
Bao pekee la Mgambo JKT walioanza ligi hiyo kwa kichapo kutoka kwa JKT Ruvu, lilifungwa dakika ya 62 na mtokea benchi, Fully Maganga.
Ni kipigo cha pili vijana hao wa Ilalala, Dar es Salaam wakitoka kulimwa mabao 5-1 na mabingwa watetezi, Yanga.

Matokeo mengine
Mbeya City 2-1 Ruvu Shooting
Mtibwa Sugar 1-0 Kagera Sugar
Azam 2-0 Ryno Rengers
JKT Ruvu 3-0 Prisons

No comments:

Post a Comment