Thursday, August 15, 2013

Surez aamua kubaki Liverpool

Surez aamua kubaki Liverpool
HATIMAYE nyota wa kimataifa wa Uruguay, Luis Suarez ametamka bayana kuwa ameamua kubaki Liverpool kutokana na mpango wake kutaka kuondoka kugubikwa na mizengwe ikiwemo kubaniwa na klabu yake ya Liverpool inayotaka abaki.
Licha ya shauku ya nyota huyo kutaka kuondoka kutokana na kuandamwa na vyombo vya habari vya England kiasi cha kutamani kuondoka Anfield na kwenda Arsenal, amesema sasa atabaki hapo kwani Liverpool imegoma kumwachia.
Mbali ya kuandamwa na vyombo vya habari, pia Suarez alikuwa na hamu ya kutua Arsenal akitamani kucheza Ligi ya Mabingwa huku wakali hao wa Emirates wakiwa tayari kutoa pauni mil 42, Liverpoo wakatupa ofa hiyo.
Nyota huyo aliyetua Liverpool misimu kadhaa kutoka Ajax, amesema anabaki Anfield kutokana na kupendwa na mashabiki wa timu hiyo
Akizungumza na gazeti la El Observador la nchini kwao Uruguay, Suarez alisema: "Kwa sasa nimeamua kubaki kutokana na upendo wa mashabiki," alisema.
Juzi, mwandishi wa Kituo cha Televisheni cha GolTV, Martin Charquero, alikuwa wa kwanza kutangza kuwa nyota huyo alikuwa amemweleza kuwa atabaki Liverpool licha ya kutakiwa na Arsenal.
Habari hiyo ya mwandishi wa kituo hicho ilitanguliwa na ile ya nahodha wa Liverpool, Steven Gerrard akisema Suarez hatahama japo kuna presha kubwa ya Arsenal kutaka ahamie Emirates.
"Luis Suarez amenihakikishia kuwa hataondoka Liverpool kutokana na ushawishi mkubwa wa mashabiki wa," alisema Mwandishi huyo kupitia akaunti yake ya twitter.
Uamuzi huo wa Suarez ni habari njema kwa Liverpool iliyokuwa ikihaha kumbakisha na mbaya zaidi pale nyota huyo alipotaka suala hilo lichukue mkondo wa kisheria kuangalia uwezekano wa kutimkia Arsenal.
Hata hivyo, Kocha wa Liverpool Brendan Rodgers, akamtaka Suarez aombe radhi kwa klabu na wachezaji wenzake kwa kauli hiyo, vinginevyo ataendelea kufanya mazoezi kivyake katika kipindi
hiki kuelekea msimu umpya wa Ligi Kuu.
Suarez abayetumikia adhabu ya mechi sita za Ligi Kuu kwa kosa la kumng’ata Branislav Ivanovic wa Chelsea mwishoni mwa msimu uliopita, alimaliza msimu huo akifunga mabao 23, hivyo kuwa nafasi ya pili kwa ufungaji.

No comments:

Post a Comment