Sunday, July 21, 2013

Naser Chadli
Spurs yanasa saini ya Chadli
KLABU ya Tottenham imethibitisha kumsajili nyota wa kimataifa wa Ubelgiji, Naser Chadli kutoka klabu ya  FC Twente kwa ajili ya msimu ujao.
Winga huyo mweye umri wa miaka 23, tayari jana alikuwa mjini hapa kukamilisha taratibu za kujiunga na klabu hiyo akifuata nyayo Wabelgiji wenzake, Mousa Dembele na Jan Vertonghen.
Chadli, anayecheza pia kama winga wa pembeni, ni mchezaji wa pili kusajiliwa Spurs akitanguliwa na  Mbrazil, Paulinho kutoka Corinthians aliyegharimu kiasi cha pauni mil 20.
Baada ya kukamilisha taratibu zote, ataungana na kikosi cha Kocha Andre Villas-Boas kilichopo Hong Kong kujiandaa na msimu mpya.

No comments:

Post a Comment