Tuesday, July 30, 2013

Messi atwaa tuzo Ulaya
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Argentina anayecheza katika klabu ya FC Barcelona ya hapa, Lionel Messi, amefurahia kutwaa tuzo ya nyota aliyefunga zaidi ya mabao 50 kwa msimu uliopita.
Messi ambaye pia anashikilia rekodi ya kuwa nyota bora wa dunia
mara nne mfululizo, ametwaa tuzo hiyo kwa mara ya tatu akiwabwaga mkongwe Gerd Muller aliyewahi kufunga mabao 85, rekodi ambayo  ilidumu kwa miaka 40
Katika msimu uliopita, Messi (26), aliivunja rekodi hiyo kwa kufunga mabao 91 kati ya 313 yaliyofungwa na timu yake kwa msimu.
Kwa upande wa Messi, si mara ya kwanza kutwaa tuzo hiyo kwani alifanya hivyo pia katika miaka ya 2009 na 2011.
Nyota wengine waliowahi kutwaa tuzo hiyo kwa kufunga mabao mengi kwa msimu, ni Cristiano Ronaldo (2008), Wesley Sneijder (2010), na Cristiano 2012.
Mbali ya kufunga mabao mengi, Machi mwaka huu Messi aliweka rekodi ya kufunga mabao katika mechi 19 mfululizo La Liga, ikiwa ni rekodi ya ya aina yake katika ligi kuu.
Baada ya kutwaa tuzo hiyo, Messi alisema: “Nimefurahi sana kwa mafanikio haya. Kama wachezaji,  tulifanya kazi kubwa kuipatia heshima timu, tuzo hii haikustahili kuja kwangu, bali kwa timu nzima.”
Tuzo hiyo ambayo imekuwa ikiratibiwa na mtandao wa Goal, mshindi amekuwa akipigiwa kura na waandishi wa habari wapatao 500 kwa kushindanisha nyota bora 50.

No comments:

Post a Comment