Wednesday, July 31, 2013

Beckham kumiliki timu Marekani
Beckham (kulia) akiwa pamoja na Ronaldo walipokutana jijini, Los Angeles, Marekani
NYOTA wa zamani wa Los Angeles Galaxy ya Ligi Kuu ya Marekani, David Beckham, anakaribia kutangazwa kuwa mmiliki na bosi mpya wa klabu jijini Miami.
Becks, 38, ana chaguo linalomruhusu kununua hisa katika timu ya Ligi Kuu ya Marekani ‘Major League Soccer – MLS’ baada ya kuichezea LA Galaxy na sasa yuko katika nafasi ya kutumia nafasi hiyo.
Mkataba wa Beckham na Galaxy ulikuwa na kipengele kinachomuwezesha nyota huyo kuanzisha ama kumiliki klabu katika Ligi Kuu kwa dau linaloanzia dola za Marekani milioni 25.
Beckham ameripotiwa mara kadhaa kukutana na bilionea raia wa Bolivia, Marcelo Claure, ambaye amedhamiria kuamua na nyota huyo wa zamani wa Man United na Real Madrid, kuhusu uanzishwaji wa timu mpya na uwanja mpya.
Mkuu wa MLS, Don Garber, alisema: “Sisi tunadhani itakuwa kali David Beckham kushiriki katika ligi yetu. Tutaendelea kujadiliana naye kwa uhakika kuhusu hilo.”
Beckham alistaafu kuichezea LA Galaxy baada ya kumalizika kwa msimu uliopita, alioiwezesha kuipa klabu hiyo ubingwa wa Ligi Kuu.

No comments:

Post a Comment