Tuesday, September 24, 2013

Van Persie kuwakosa Liverpool kesho

Van Persie kuwakosa Liverpool kesho
KOCHA wa Man United, David Moyes amesema hatomjumuisha kikosini mshambuliaji wake Robin Van Persie kwenye mechi ya Kombe la Ligi kati yao na Liverpool.
Van Persie atalazimika kuikosa mechi ya pili mfululizo baada ya kuumia katika mazoezi muda mchache kabla ya mpambano na wapinzani wao wa jadi Manchester City mchezo uliopigwa mwishoni mwa wiki iliyopita kwa kuangukia pua kwa mabao manne kwa moja kutoka watani wao.
"Sifikiri kama Robin Van Persie atacheza siku ya Jumatano na Liverpool, ila anaweza kucheza siku ya Jumamosi katika mechi ya ligi na Timu ya West Brom." amesema Moyes

No comments:

Post a Comment