Tuesday, September 24, 2013

Carlo Ancelotti ajifariji kwa Mesut Ozil

Carlo Ancelotti ajifariji kwa Mesut Ozil
MABAO 15 yaliyofungwa na Real Madid katika mechi nne za mwisho, yamempa kiburi kocha Carlo Ancelotti akisema hawezi kumkumbuka Mesut Ozil aliyetimkia Arsenal ya England.
Ancelotti anasema hana sababu ya kufanya hivyo kutokana na kazi nzuri inayofanywa na Coentrao na Varane katika kikosi hicho, mabingwa mara tisa wa Ulaya.
Anaamini kuondoka kwa Mesut Ozil kwenda Arsenal, bado hakujaathiri uwezo wa kikosi chake dimbani, akijivunia ushindi wa kishindo wa 6-1 dhidi ya Galatasaray 6-1 katika Ligi ya Mabingwa Ulaya na 4-1 dhidi ya Getafe.

No comments:

Post a Comment