Tuesday, July 23, 2013

Martino amrithi Vilanova Barca
Gerardo Martino
KOCHA Gerardo Martino amepewa mkataba wa miaka miwili kuinoa Barcelona akichukua nafasi ya Tito Vilanova aliyejiuzulu kwa sababu za kiafya.
Martino maarufu kama Tata, ametua Camp Nou kwa ushawishi mkubwa wa Mkurugenzi wa Michezo wa klabu hiyo, Andoni Zubizarreta aliyezungumza naye kabla ya jana kutangazwa rasmi.
Tata aliondoka Hispania tangu juzi kwenda Hispania kwa mazungumzo kabla ya kusaini mkataba kubeba mikoba ya Vilanova aliyejiuzulu Ijumaa iliyopita kujipa muda zaidi wa kupigania afya yake.
Vilanova aliyekuwa amechukua nafasi ya Pep Guardiola mwaka mmoja uliopita, amekuwa akisumbuliwa na maradhi ya kansa ya koo ambapo mara kadhaa amekuwa akitibiwa na kupata nafuu ya muda.
Tata (50), atasaidiwa na kocha wa viungo, Elvio Paolorroso na Kocha Msaidizi, Jorge Pautasso, ametwaa nafasi hiyo akimpiku kiungo wa zamani wa timu hiyo, Luis Enrique aliyekuwa akitajwa.
Martino ni Muargentina wa nne kuinoa Barcelona, akitanguliwa na Helenio Herrera, Roque Olsen na Cesar Luis Menotti.
Nje ya ukocha, Enrique ataungana na Muargentina mwenzake, Lionel Messi nyota mahiri katika kikosi hicho ambacho kitaingia kwenye msimu mpya wa La Liga kama bingwa mtetezi.
Jumatatu hii Messi alizungumza na Tata aliyewahi kuinoa Newell na Paraguay na kaka yake Matias Messi na kumpongeza Martino kwa jukumu jipya Camp Nou.

"Karibu Tata!!" aliandika Messi kupitia Twitter. " Naamini utaendelea kupata mafanikio ukiwa hapa!! Asante Tito!! Mungu akubariki!!"

No comments:

Post a Comment