Tuesday, July 23, 2013

Cameroon yafutiwa kibano
SHIRIKISHO la soka la Kimataifa (Fifa) imekiondolea kifungo chama cha soka cha Cameroon
(FECAFOOT) baada ya matakwa yake ya kutaka kuundwa Kamati ya Mpito kuelekea uchaguzi mkuu, kutekelezwa.
Julai 4, mwaka huu, Fifa walisimamisha uanachama wa Cameroon baada ya serikali ya nchi hiyo kuingilia uendeshaji wa soka wa Fecafoot, hivyo ikaagiza kuundwe Kamati kwa sharti kuwa atakayekuwemo huko asiwe na ndoto ya kugombea uchaguzi ujao.
Chini ya kifungo hicho, Caneroon iliondolewa kwenye kampeni ya kupigania tiketi ya Kombe
la Dunia nchini Brazil ambapo Septemba itacheza na Libya kuwania hatua ya 10 bora itakayotoa tano za kwenda Brazil mwakani.
Cameroon ndio kinara wa kundi I, ikiwa na pointi 10 ikifuatiwa na Libya yenye pointi tisa huku DR Congo ikiwa ya tatu kwa pointi sita na Togo ya mwisho kwa pointi moja iliyovuna katika mechi tano.
Kwa msinamo wa kundi hilo, mechi baina ya Cameroon na Libya ndio itaamua timu ya kutinga hatua ya 1o bora ingawa Cameroon itakuwa ikihitaji walau sare tu kusonga mbele wakati Libya ikihitaji ushindi.
Juzi, Fifa ilitoa taarifa kuwa imeridhia na utekelezwaji wa maagizo yake kwa FECAFOOT, hivyo inaondoa kifungo na kuwataka kuendelea na mchakato zaidi wa kuelekea kwenye uchaguzi chini ya vyomvyo husika wakiwemo Fifa (Primo Cavaro) na Shirikisho la soka Afrika (CAF).
Mgogoro wa soka ulitokana na Rais wa FECAFOOT Iya Mohammed kushinda katika uchaguzi mkuu uliofanyika hivi karibuni licha ya kuzuiwa kutokana na tuhuma za matumizi mabaya ya fedha.
Cameroon ilipata nguvu baada ya kupewa pointi tatu za Togo kwa kosa la kumchezesha Alaixys Romao ambaye si raia katika mechi ya Juni 9.
Licha ya Cameroon kufungwa 3-0, wamepewa ushindi hivyo wana pointi 0, hivyo kuhitaji walau pointi moja kutinga hatua ya 10 bora.

No comments:

Post a Comment