Monday, September 9, 2013

Serena atetea taji la US Open

Serena Williams atetea taji la US Open
NYOTA namba moja kwa ubora wa tennis kwa wanawake, Serena Williams, ameseka kama angeshindwa kutetea ubingwa wa michuano ya US Open ukiwa wa tano katika historia yake, mwaka 2013 ungekuwa mbaya kwake.
Serena (31), juzi alitetea taji akimshinda Victoria Azarenka raia wa Belarus kwa 7-5 6-7 (6-8) 6-1, likiwa taji lake la pili la kimataifa kwa mwaka huu, akianza na French Open.
Aidha, Williams amefikisha taji la 17 la kimataifa katika historia yake kama ilivyo kwa Roger Federer, raia wa Uswis ambaye ni nyota namba saba kwa ubora.
Pia, kwa ushindi wa jana, Serena ameweka rekodi ya kushinda mechi 34 kwa mwaka huu wa 2013.
"Licha ya kutwaa ubingwa wa French Open, kama nisinngetetea ubingwa wa US Open, mwaka huu ungekuwa mbaya kwangu.
"Mambo yaliniendea vizuri katika fainali hii ya US Opena kuliko ilivyokuwa French Open.
Hata hivyo, pamoja na Azarenka ambaye ni nyota namba mbili kwa ubora kufungwa mechi hiyo, alionesha upinzani mkubwa kwa Serena aliyetumia mbinu na uzoefu zaidi kupindua matokeo hayo na kuibuka mshindi.
Kwa Azarenka ni bahati mbaya kwake kufungwa katika fainali ya michuano hiyo kama ilivyokuwa mwaka jana alipofungwa pia na Serena.

No comments:

Post a Comment