Tuesday, July 30, 2013

Maradona atoa dozi kwa mpiga picha
Maradona (kulia) akimshambulia kwa mateke mpiga picha
MPIGA picha wa jarida maarufu amefungua jalada kituo cha polisi, akimtuhumu nguli wa zamani wa soka la hapa Diego Maradona kumshambulia kwa mateke kinenani katika tukio tata lililoacha maswali.
Mpiga picha huyo wa kiume aitwaye Enrique Medina, ameripoti kushambuliwa na mkongwe huyo Jumapili usiku akiwa nje ya nyumba ya baba yake Maradona, wakati alipoweka kambi ya muda kusubiri kumpiga picha mshindi huyo wa Kombe la Dunia 1986.
Medina aliliambia Shirika la Habari la Associated Press Jumatatu kuwa Maradona alikimbia kana kwamba ‘anayeenda kupiga mpira wa adhabu ndogo,’ na kisha akampiga yeye teke kali kinenani na juu ya mguu na kumsababishia maumivu makali.
“Halikuwa teke la mtu wa kawaida,” alisema Medina na kuongeza: “Lilikuwa teke kutoka kwa mtu anayejua hasa kupiga mateke ... Alionekana kuwa na hasira hasa, aliyekosa utu kwa muda. Lilikuwa ni tukio lililotokea katika nyumba ya baba yake.”
Mara kadhaa Maradona amevilalamikia vyombo vya habari kuwa vinamfuatilia sana hadi maisha yake ya ndani. Mwaka 1994, aliwahi kuwafyatulia risasi hewani wanahabari na kujikuta akifungiwa miaka miwili wakati huo akiichezea Newlle’s Old Boys.
Mei mwaka huu, Maradona aliwahi kuliacha gari katika barabara kuu na kuokota mawe na kuanza kuwarushia wapiga picha waliokuwa wakimfuatilia kutoka Uwanja wa Ndege kwenda nyumbani kwao.
Tukio la juzi, limetokea wakati Maradona aliporejea Argentina kutoka Dubai anakofanya kazi kama Balozi wa Soka Falme za Kiarabu.

No comments:

Post a Comment