Thursday, September 12, 2013

Ozil: Sikuthaminiwa Santiago Bernabeu

Ozil: Sikuthaminiwa Santiago Bernabeu
MCHEZAJI Mesut Ozil, amekana kauli ya Rais wa Klabu ya Real Madrid, Florentino Perez, kwamba ameondoka kutokana na kukosa vigezo za nyota wa kimataifa.
Mbali ya kukana hilo, Ozil amesema kilichomwondoa ni kukerwa na kutopewa heshima yake Real Madrid licha ya kuwa katika kiwango bora kiuchezaji.
Ozil ameyasema hayo wakati baba yake mzazi akiwa kwenye harakati za kuchukua hatua za kisheria dhidi ya Perez kwa kauli yake dhidi ya mwanaye.
Kwa mujibu wa Peres, Ozil alikuwa akitumia muda mwingi kujirusha na wasichana na kukesha kwenye baa.
Hata hivyo, nyota huyo wa kimataifa wa Ujerumani, hakupenda kuingia kwenye vita ya maneno na Perez, akiishia kusema aliondoka kutokana na kutothaminiwa.
"Sitaki kusema lolote baya dhidi ya Real Madrid kwa sababu miaka yangu mitatu pale ilikuwa ya mafanikio.
"Tulibeba mataji na niliisha kwa furaha, kila aliyenifahamu, alitambua mchango wangu kwa Real Madrid.
"Nikiwa pale nilicheza mechi 159, katika mazingira ya kawaida, huwezi kucheza mechi nyingi hivyo kama hupo katika kiwango bora.
"Tatizo sikupata heshima niliyostahili kulingana na mchango wangu. Nilikuwa kwenye mazingira magumu na nilipozungumza kwa simu na Kocha wa Arsenal (Arsene Wenger), alionesha kuniheshimu."
Ozil aliyewahi pia kukipiga Werder Bremen ya Ujerumani, anaamini kutua kwake Arsenal, kutaboresha zaidi kiwango chake.

Bale amuweka kando C.Ronaldo katika utambulisho wa jezi mpya Real Madrid

Bale amuweka kando C.Ronaldo kwenye utambulisho wa jezi mpya Real Madrid



TFF yatoa vibali kwa nyota wa Tanzania

TFF yatoa vibali kwa nyota wa Tanzania

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limetoa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa nyota wawili wa Tanzania kucheza soka chini Afrika Kusini.
Nyota hao ni Robert Kobelo na Mohamed Ibrahim wamepewa hati hizo baada ya kuombewa na Chama cha Mpira wa Miguu Afrika Kusini (SAFA) kama wachezaji wa ridhaa ili wajiunge na klabu ya Cacau United ambayo timu yake inacheza Ligi Daraja la Pili katika Wilaya ya Cacau.
Naye mchezaji Said Maulid aliyejiunga na Ashanti United akitokea nchini Angola msimu huu amepata ITC ambayo sasa inamwezesha kuchezea timu hiyo katika mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inayoingia mzunguko wake wa tatu kesho.

Ozil aanza rasmi mazoezi Arsenal

Mesut Ozil aanza rasmi mazoezi Arsenal
MCHEZAJI mpya wa Arsenal, Mesut Ozil ameyaanza maisha mapya ya Ligi Kuu England kwa mara ya kwanza tangu asajiliwe akitokea Klabu ya Real Madrid.
Ozil ameoneka akiwa katika mazoezi ya pamoja na wachezaji wenzake wa Arsenal kwenye uwanja mazoezi.
Kiungo huyo ambye ameweka rekodi ya usajili wa bei ghali ya paundi milioni £42.5 (sawa na fedha za Kitanzania bilioni 108. 5