Saturday, July 20, 2013

Utd yazidi kumtolea macho Cesc Fabregas

PAMOJA na Makamu Raia wa Barcelona,  Josep Maria Bartomeu, kusema kamwe kiungo wao Cesc Fabregas hauzwi, Klabu ya Manchester United imeongeza kasi ya kumngoa Santiago Bernabeu.
Kocha wa United, David Moyes, aliyasema hayo jana baada ya timu yake kushinda 5-1 katika mechi ya kirafiki dhidi ya A-League All Stars.
Alitumia nafasi hiyo kusisitiza kuwa, United imewasilisha ofa ya pauni mil 30, hivyo wanasubiri jibu kutoka Barcelona.
Wakati United ikiwa na mipango hiyo, nyota wake mahiri Robin van Persie, alisema jana anamkaribisha Fabregas kwa mikono mwili.
“Ni mchezaji mzuri,” alisema Fabregas alipozungumza na Channel Seven, licha ya kukiri hajawahi kuzungumza naye. 

No comments:

Post a Comment