Tuesday, September 3, 2013

Manywele Fellaini atua rasmi Man United

Manywele Fellaini atua rasmi Man United
Fellaini akikabidhiwa jezi yenye namba 31 mgongoni
KIUNGO mahiri Marouane Fellaini amefanikiwa kujiunga na Mabingwa wa England Manchester United, dakika za majeruhi kabla ya dirisha la usajili halijafungwa.
Felllaini aliyesajiliwa muda wa saa 5:06 za usiku kwa masaa ya England na kumwaga wino wa kuitumikia United kwa mkataba wa miaka mitano wenye thamani ya paundi milioni £27.5.
Kwa kiasi hicho cha fedha 'Bwana Manywele' ameingia kwenye orodha ya wachezaji waliosajiliwa United kwa mshiko mkubwa kama vile, Wayne Rooney,Dimitar Berbatov, Rio Ferdinand na Juan Sebastian Veron.
Wakati huo huo kunataarifa ambazo hazikuthibitishwa na Klabu ya Man Utd kuwa wamefanikiwa kumsajili kwa mkopo Beki wa kushoto wa Real Madrid, Fabio Coentrao.