Monday, July 29, 2013

Man Utd kula matapishi ya Pogba
TOVUTI moja ya Kihispania imetoa taarifa ya mshangao kuwa aliyekuwa kiungo wa Man United Paulo Pogba kwamba anaweza akarejeshwa Old Trafford.
Mfaransa huyo alijiunga na Juventus msimu wa mwaka jana majira ya joto.
Hata hivyo, Juve wanaripoti wazi kwamba Juve hawana nia ya kusikiliza ofa inayotolewa kwa ajili ya kiungo huyo.
Pogba aliondoka United kwa sababu ya kukosa nafasi ya kucheza kikosi cha kwanza.
Hivyo wataelekeza nia yao ya kumsajili Pogba endapo watakosa huduma ya Fabregas ambaye Kocha wa Man Utd amesema hawatoongeza tena ofa kwa kiungo huyo wa Barcelona.

No comments:

Post a Comment