Thursday, July 25, 2013

Guardiola awapiga wanae 2-0
Baadhi ya wachezaji wa Bayern wakinyanyua kombe
KOCHA Mkuu wa Bayern Munich Pep Guardiola ameifunga klabu yake ya zamani Barcelona kwa ushindi wa goli 2-0 katika mechi ya kirafiki iliyopigwa ndani ya dimba la Allianz Arena, jijini Munich.
Philipp Lahm ndiye aliyefungua kalamu ya mabao hayo katika dakika ya 14 goli hilo lililodumu kwa muda mrefu mpaka ilipofika dakika 87 Mshambuliaji wao hatari Mario Mandzukic akashindilia msumari wa mwisho.
Timu hizo hii ndiyo mechi yao ya kwanza tangu walipokutana kwenye mchezo wa nusu fainali ya Kombe la Mabingwa wa Ulaya, ambao mechi hiyo Barcelona walikubali kipigo cha Mbwa Mwizi cha mabao 7-0.

No comments:

Post a Comment