Friday, July 19, 2013

Keshi amwita Ameobi kuivaa Bafana Bafana

KOCHA wa timu ya taifa ya Nigeria, Stephen Keshi amemwita mshambuliaji wa kimataifa Shola Ameobi anayekipiga Newcastle United ya England kwa ajili ya mechi maalumu dhidi ya Bafana Bafana kwa heshima ya Mzee Nelson Mandela ambaye juzi alitimiza umri wa miaka 95. 
Keshi amemwita Ameobi kwa mechi hiyo itakayofanyika Agosti 14, mjini Durbun ambapo kutapigwa michuano maalumu ya Nelson Mandela Challenge.
Kuitwa kwa nyota huyo ni baada ya kumalizana na klabu yake ya Newcastle United kuhusu hatima ya mkataba wake ambao awali ulikuwa ukimzuia kuichezea timu hiyo ya taifa katika michuano ya Kombe la Afrika iliyochezwa mapema mwaka huu nchini hapa ambapo walitwaa ubingwa kwa kuwafunga Burkina Faso.
Kocha huyo aliamua kumpigania mchezaji huyo alitaka kuimarisha kikosi chake baada ya kuyumba katika mechi kadhaa kutokana na pengo la Emmanuel Emenike na Victor Moses ambao walikuwa majeruhi.
Baada ya kupona, Emenike na Moses watakuwemo kwenye kikosi hicho cha nyota 20 huku kipa waa muda mrefu Vincent Enyeama akiachwa baada ya nafasi yake kuzibwa na Obinna Nsofor na Uche Nwofor aliyeitwa kwa mara ya kwanza.
Naye Ogenyi Onazi anayecheza katika klabu ya Lazio ya Italia, amerejeshwa kwenye kikosi cha timu hiyo baada ya kushindwa kwenda nchini Brazil kwa michuano ya Kombe la Mabara kutokana na kuwa majeruhi.
Wachezaji hao na timu zao kwenye mabano ni:-
Makipa: Austin Ejide (Hapoel Be’er Sheva, Israel); Chigozie Agbim (Enugu Rangers, Nigeria)
Mabeki: Kenneth Omeruo (Chelsea FC, England); Efe Ambrose (Celtic FC, Scotland); Godfrey Oboabona (Sunshine Stars, Nigeria); Azubuike Egwuekwe (Warri Wolves, Nigeria); Elderson Echiejile (Sporting Braga, Ureno)
Viungo: Mikel Obi (Chelsea FC, England); Fegor Ogude (Valerenga FC, Norway); Victor Moses (Chelsea FC, England); John Ogu (Academica de Coimbra, Ureno); Ogenyi Onazi (SS Lazio, Italy); Nnamdi Oduamadi (AC Milan, Italia); Sunday Mba (Enugu Rangers, Nigeria).

Washambuliaji: Ahmed Musa (CSKA Moscow, Russia); Brown Ideye (Dynamo Kyiv, Ukraine); Shola Ameobi (Newcastle United, England); Emmanuel Emenike (Spartak Moscow, Russia); Obinna Nsofor (Lokomotiv Moscow, Russia); Uche Nwofor (VVV Venlo, Uholanzi)

No comments:

Post a Comment