Saturday, July 20, 2013

Gerardo Martino ‘Tata’
Gerardo kumrithi Vilanova
KOCHA wa zamani wa timu ya taifa ya  Paraguay, Gerardo Martino ‘Tata’ anapewa nafasi kubwa ya kuziba nafasi ya Tito Vilanova, aliyejiweka kando kutokana na sababu za kiafya.
Vilanova (44), aliyekuwa ametwa nafasi hiyo baada ya kuondoka kwa Pep Guardiola, amekuwa akisumbuliwa na kansa ya koo kwa muda mrefu.
Kuna habari kuwa, Martino mwenye umri wa miaka 50, alitarajiwa kwenda nchini Hispania kwa mazungumzo ya kazi hiyo.
Martino, aliyeipa Newell's Old Boys ubingwa wa Argentina msimu uliopita, kwa sasa yupo nje ya mkataba na wakali hao.
Ni kocha mwenye rekodi ya kubeba ubingwa wa Paraguay na mwaka 2007, alitwaa tuzo ya Kocha Bora Amerika Kusini.

Kocha huyo aliyezaliwa Novemba 20, 1992, pia amewahi kufundisha Brown de Arrecifes, Platense, Instituto, Libertad, Cerro Porteño, Colón, Libertad na timu ya taifa ya Paraguay kuanzia 2006 hadi 2011.

No comments:

Post a Comment