Friday, July 19, 2013


Titi Vilanova

Kansa yamuachisha kazi Vilanova

 KLABU ya Barcelona imezungumza na wanahabari na kuwambia kwamba kocha wake Tito Vilanova ameacha kazi kutokana na kusumbuliwa na maradhi ya kansa ya koo.
Vilanova, ambaye alijiunga Nou Camp akichukua nafasi ya Pep Guardiola katika msimu uliopita, lakini mwaka 2011, alijikuta akisumbuliwa na maradhi ya kansa.
Maradhi hayo yalionekana kukua kila uchwao hali iliyosababisha Desemba kufanyiwa upasuaji katika tezi yake kabla ya kuanza matibabu kwenye kituo cha mionzi cha New York.
Mwaka huu tatizo limekuwa kubwa hali iliyosababisha kufanyiwa matibabu makubwa ikiwa ni pamoja na kuwa na mwangalizi.
Katika mkutano huo wa wanahabari uliohudhuliwa pia na wanachama wa klabu hiyo, Rais wa Barca, Sandro Rosell alisema "Habari ambayo ninayo ni kuhusu jambo nisilohitaji kuwaeleza.
“Baada ya kutathmini juu ya Tito na kumfanyia vipimo nasikitika kuwaambia kwamba hataweza kuwa kocha chaguo la kwanza.
Baadhi ya wachezaji waliohudhulia mkutano huo alikuwa mchezaji Lionel Messi na baadhi ya wachezaji wengine.
Akizungumzia kuhusu kama klabu hiyo itatafuta kocha mwingine katika siku za hivi karibuni.
"Tutatangaza jina la kocha mpya wa FC Barcelona mapema wiki ijayo," Rosell aliongeza katika maelezo yake.
Tetesi kutoka Hispania zinasema kuwa huenda kati ya makocha hawa watapewa timu hiyo ambao ni Joan Francesc Ferrer ‘Rubi’, na kocha wa Tottenham, Andre Villas-Boas.

No comments:

Post a Comment