Saturday, July 20, 2013

Mshambuliaji wa Simba, Marcel Boniventure akitafuta mbinu za kumtoka beki wa URA ya Uganda, Walulya Derrick.
Simba yanyofolewa sharubu U/Taifa 
TIMU ya Simba jana ilichapwa mabao 2-1 katika mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya URA ya Uganda iliyochezwa Uwanja wa Taida, jijini Dar es Salaam.
Shujaa kwa upande wa URA, alikuwa Lutimba Yayo aliyeifungia mabao yote katika dakika za 54 na 74, hivyo kuanza vema ziara yao ya mechi za kirafiki ambapo leo itacheza na Yanga.
Simba walitangulia kupata bao dakika ya saba, likifungwa na Betram Mombeki akitumia uzembe wa mabeki wa URA kukawia kuokoa mpira karibu ya lango.
Simba: Abel Dhaira, Nassor Masoud Chollo, Issa Rashid, Samuel Senkoom, Rashid Juma, Jonas Mkude, Ramadhan Singano, Wlliam Lucian, Betram Mombeki, Zahor Pazi na Marcel Boniventure.
URA: Bwete Brian, Walulya Derrick, Munaaba Allon, Owino Joseph, Mugabi Jonathan, Agaba Oscar , Feni Ali, Ngama Emmanuel, Lutinga Yayo, Kasibanto James na Mugabi Yasin.
Waganda hao leo wanashuka tena dimbani kucheza na mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga kwenye Uwanja whuo wa Taifa, jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment