Monday, July 29, 2013

Newcastle yanawa mikono kwa Gomis
Bafetimbi Gomis
TIMU ya soka inayoshiriki Ligi Kuu England imejitoa katika mbio zake za kumsajili mshambuliaji raia wa Ufaransa anayeichezea klabu ya Lyon, Bafetimbi Gomis.
Loic Remy
Imefahamika Newcastle waliongeza ofa yao kwa mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27 ya paundi milioni 6.9
Hata hivyo upande wa Klabu yake ya Lyon waliikata ofa hiyo wakitaka waongezwe.
Kocha wa Newcastle, Alan Pardew amekuwa na hamu ya kuongezea makali katika safu yake ya ushambuliaji kwa kumsajili Gomis ambaye alifunga mabao 18 katika msimu ulioisha kwa Lyon.
Kwa sasa ameelekeza nguvu yake yakutamani kumsajili mshambuliaji wa QPR Loic Remy kwa mkopo wa  muda mrefu.
Japokuwa anasafu kali ya ushambuliaji inayoongozwa na Waafrika, Shola Ameobi na Papiss Cisse lakini Pardew na uongozi wa klabu yake wanafanya kazi ya kuhakikisha wanaleta sura mpya kwenye klabu hiyo

No comments:

Post a Comment