Friday, July 26, 2013

Barca yaitaabisha Man Utd kwa Fab
NDOTO za Klabu ya Manchester United kupata saini ya kiungo Cesc Fabregas, zimeyeyuka baada ya FC Barcelona kusisitiza kwa mara nyingine kuwa hawamtoi Camp Nou.
Licha ya Manchester United kugonga mwamba mara ya kwanza katika kumwania nyota huyo, bado ilituma ofa kwa mara ya pili ya pauni mil 30 na mchezaji. 
Makamu Rais wa Klabu hiyo, Josep Maria Bartomeu amewajibu Manchester United, kuwa hawapo tayari kumuuza kiungo huyo kwa bei yoyote.
Japo Alhamisi wiki hii Kocha wa United, David Moyes, alisema wanaendelea na juhudi za kumwania, lakini wameelezwa kuwa waachane na bishara hiyo.
Bartomeu said: "Man United imekuwa ikimtaka Fabregas kwa muda mrefu kwa sababu ni mchezaji mkubwa, lakini hauzwi
Fabregas aliyecheza soka ya utoto katika klabu ya Barcelona kabla ya kutimkia Arsenal mwaka 2003, aliondoka Emirates Agosti 2011 na kurejea Camp Nou kwa kitita cha pauni mil 30.
Akiwa Arsenal, mechi yake ya kwanza ilikuwa ya Kombe la Ligi dhidi ya Rotherham United ya Oktoba, 2003, wakati huo akiwa na umri wa miaka 16 na siku 177.
Tangu arejee Barcelona, Fabregas amekuwa hana raha kutokana na kukosa uhakika wa kikosi cha kwanza hadi kutamani kuondoka, lakini kuondoka kwa Thiago kumeongeza thamani yake Camp Nou.
Ni mara ya kwanza kwa Bartomeu kuonekana hadharani akizungumza akiwa na kocha mpya
Gerardo Martino aliyeziba nafasi ya Tito Vilanova.
Ndoano ya kwanza ya Man United kwa kiungo huyo ilikuwa Julai 15, walipokuwa tayari kucheua kiasi cha pauni mil 25 ambazo zilikataliwa kabla ya kupanda hadi 30 na mchezaji.
Tangu arejee Barcelona, Fabregas amecheza mechi 96 zikiwemo 60 za La Liga, lakini amekuwa akifunikwa na uwepo wa nyota wengine kama Xavi (33) na Andres Iniesta (29). 

No comments:

Post a Comment