Thursday, September 19, 2013

Real Madrid kuwatoa Khedira Benzema ili wampate Aguero

Real Madrid kuwatoa Sami Khedira,
Karim Benzema ili wampate Aguero
KLABU ya Real Madrid imepanga kuto ofa kwa wachezaji Karim Benzema na Sami Khedira kwa ajili ya kumchukua Sergio Aguero wa Manchester City.
Real Madrid imepanga kuwatoa sadaka wachezaji hao kwa mpigo kwa ajili ya kubadilishana na mchezaji wa Manchester City Sergio Aguero.
Akizungumzia hilo katika mtandao wa Daily Star, klabu hiyo inayoshiriki Ligi kuu ya La Liga imedhamiria kumtwaa Aguero kwa kuwatoa wakali wao, Karim Benzema na Sami Khedira.
Benzema ametajwa kutakiwa pia na Arsenal katika kipindi cha kiangazi Klabu ya Arsenal ambayo imeandaa dau la Euro milioni 40.

No comments:

Post a Comment