Friday, July 19, 2013

Zambia, Zimbabwe fainali Cosafa
ZAMBIA ambao ni wenyeji wa Kombe la Cosafa wametinga fainali ya michuano hiyo baada ya kuwafunga Afrika Kusini katika mechi ya nusu fainali iliyochezwa Jumatano, hivyo watacheza 
na mabingwa watetezi Zimbabwe wikiendi hii. 
Wenyeji hao walitinga fainali kwa ushindi wa mikwaju ya penalti baada ya kutoka sare katika muda wa kawaida ambapo Zambia walipata mikwaju yote huku shuti ya Lerato Chabangu wa Afrika ikipanguliwa na Danny Munyau. 
Zambia sasa itakutana na Zimbwabwe ambapo timu hizo zitakuwa na kumbukumbu ya fainali ya michuano hiyo ya mwaka 2009, baada ya Zimbwabwe kuifunga Lesotho mabao 2-1.

No comments:

Post a Comment