Friday, July 19, 2013

Misri, Cameroon zafumua ratiba Caf 
KAMPENI ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika inayoendelea mwishoni kwa wiki hii, imeingia dosari kutokana na mechi moja kuahirishwa na nyingine zikiwa kwenye hatihati kuchezwa kutokana na sababu kadha wa kadha.  
Mechi mojawapo iliyoindia doa ni kati ya Coton Sport ya Cameroon na Sewe Sports ya Ivory Coast za kundi B ambayo imesitishwa kwa wiki moja kupisha maridhiano kati ya Shirikisho 
la soka la Cameroon (Fecafoot) na Shirikisho la soka la Kimataifa (Fifa).
Hivi karibuni, Fecafoot ilisimamishwa uanachama na Fifa kutokana na Waziri wa Michezo 
kuingilia kati uendeshaji wa shughuli za soka, hivyo mechi hiyo haiwezi kuchezwa hadi 
pande hizo mbili zitakapopata suluhu ya mvutano uliopo.    
Mechi nyingine iliyopo kizani ni kati ya Zamalek na Al Ahli za Misri ambazo zilikuwa 
zicheze leo mjini Cairo katika hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho ambayo sasa 
itachezwa kesho.  
Shirikisho la soka Afrika (Caf), lilisema kuwa hadi kufikia jana, walikuwa wakijadiliana 
na Chama cha soka cha Misri (EFA) huku kukiwa na habari kuwa, viongozi wa EFA 
wanahofia athari ya mapato kutokana na mabadiliko hayo.
Hata hivyo, kumekuwa na mkanganyiko kuhusu lini mechi hiyo itachezwa kwani Ahly 
Kupitia mtandao wao wanasema mechi hiyo itachezwa kati ya Jumanne au Jumatano 
huku taarifa ya Zamalek ikisema mechi hiyo ni Jumatatu au Jumatano.
Kauli hizo mbili tofauti juu ya lini hasa mechi hiyo itachezwa, imeleta mkanganyiko 
mkubwa japo inajulikana wazi sasa itachezwa mjini  El Gouna huku mashabiki wengi 
wakiwa na hofu ya kuzuka vurugu.
Aidhga, kutokana na uwanja huo kutokuwa na taa za kutosha, mechi hiyo imepangwa kuanza mapema. 
Kwa upande wa mechi ya Coton Sport na Sewe Sports iliyokuwa ichezwe leo, imesogezwa hadi Julai 27 kutoa nafasi kwa Fecafoot na Fifa kumaliza mgogoro uliopo.  
Julai 4, Fifa iliifungia Cameroon kutokana na serikali kuingilia utendaji wa Fecafoot ikitaka kuundwe Kakati ya mpito kuendesha shughuli za soka kuelekea uchaguzi mkuu.

No comments:

Post a Comment