Friday, July 19, 2013

YayaToure

Toure amwagia sifa Tata Madiba 

KIUNGO mahiri wa timu ya Manchester City, Yaya Toure amesema ni heshima na historia ya aina yake kwake na wachezaji wengine kucheza mechi rasmi ya kuadhimisha miaka 95 ya Rais 
wa zamani wa nchini hapa, Mzee Nelson Mandela.
Toure ambaye pia ni nyota bora wa Afrika, aliyasema hayo juzi saa chache kabla ya timu yake ya Manchester City iliyopo nchini kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu ya England  kucheza mechi ya kirafiki kwa heshima ya Mandela dhidi ya AmaZulu ikiwa ya mwisho katika ziara yao.
Mechi hiyo iliyochezwa juzi jioni katika Uwanja wa Moses Mabhida ilikwenda sambamba na maadhimisho ya miaka 95 ya kuzaliwa kwa Mzee Mandela ambayo iliadhimishwa katika nchi mbalimbali za ndani na nje ya Afrika kwa kufanya shughuli za kijamii kwa dakika 67.
Walitumia dakika hizo kama ishara ya miaka 67 ya harakati za Mzee Mandela katika masuala ya kisiasa kwa kiongozi huyo wa zamani wa Afrika Kusini ambaye aliongoza kwa miaka mitano kabla ya kumpisha Thabo Mbeki na sasa Jacob Zuma.
"Ni birthday ya mzee wa Africa. Nafurahi sana na kujisikia fahari kubwa kucheza mechi hii maalumu ya kuadhimisha miaka 95. Naamini atapata nafuu haraka," alisema Toure alipozungumza na Footba ll411. 
Yaya aliyekuwemo kwenye kikosi kilichofungwa mabao 2-0 na SuperSport United wiki iliyopita, alisema wakiwa nchini hapa wamenufaika kwa kiasi kikubwa na ziara ya nchini hapa ndio maana walionesha kiwango bora walipocheza dhidi ya Usuthu. 
"Tumekuwa tikicheza kwa juhudi kubwa kujiweka fiti kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa Ligi Kuu ya England," alisema Toure na kuongeza: 
"Kwetu ni mechi muhimu sana. Nimekuwa nikifarijika kucheza na timu za Afrika kwani tunapata fursa ya kujifunza mengi." 
Toure, aliyetoa mchango mkubwa kwa Man City kutwaa ubingwa wa England msimu wa 2011/12, alisema kurejea kwa Jose Mourinho katika timu ya Chelsea na David Moyes kuino Manchester United na usajili wa nyota mbalimbali wapya, kutaongeza ugumu wa ligi hiyo msimu ujao.  
"Kurejea kwa Mourinho katika Ligi Kuu ya England na usajili wa nyota wapya huku Chelsea na Arsenal zikipambana kurejesha heshima yao, nadhani itakuwa ni ligi ya ushindani zaidi, lakini naamini tutabeba ubingwa kwa sababu tuna kikosi bora." 
Kwa mujibu wa Toure, City inajipanga kufanya vizuri katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya ikiwezekana kutwaa uningwa baada ya kuishia hatua ya makundi katika misimu miwili iliyopita.

No comments:

Post a Comment