Friday, July 19, 2013

Bongani Ndulula (kulia) wa AmaZulu akifunga bao la kwanza kwa
timu yake dhidi ya Manchester City, juzi
Man City yamaliza ziara kwa kichapo
MANCHESTER City ya England, juzi ilikumbana na kichapo kingine cha mabao 2-1 kutoka kwa AmaZulu katika mechi ya kirafiki iliyochezwa kwenye Uwanja wa Mosea Mabida, mjini hapa.
Katika mechi hiyo iliyokwenda sambamba na maadhimisho ya miaka 95 ya Mzee Nelson Mandela, Manchester City walicheza bila kocha wake Manuel Pellegrini aliyeondoka ghafla na kwenda Chile kwa matatizo ya kifamilia.
Licha ya mechi hiyo kupambwa na furaha ya timu hiyo kufanikiwa kuwasajili wachezaji Alvaro Negredo Stevan Jovetic, walishindwa kuhimili kishindo cha AmaZulu hivyo kupata kichapo kingine kama ilivyokuwa Jumapili walipofungwa mabao 2-0 na SuperSport, mjini Pretoria.
Katika mechi ya juzi, AmaZulu walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 20, likifungwa na Bongani Ndulula kabla ya Manchester City kusawazisha dakika ya 26, likifungwa na James Milner, hivyo timu hizo kwenda mapumziko zilkiwa sare ya bao 1-1.
Zikisalia dakika tatu kabla ya filimbi ya wmisho, Van Heerden aliifungia AmaZulu bao la ushindi kwa mkwaju wa penalti.
AmaZulu: Kapini; Macala, Teyise, Msekeli, Hlanti; Madondo, Madubanya, Manqana, Zondi, Dlamini; Ndulula. 
Man City: Hart/Pantilimon; Richards/Zabaleta, Kompany/Garcia, Nastasic/Lescott, Kolarov/Boyata, Milner/Razak, Toure/Rodwell, Fernandinho/Barry, Sinclair; Dzeko/Nimely, Nasri/ Suarez. 
Kuhusu kutokuwepo kwa Pellegrini, Msaidizi wake Brian Kidd alisema aliondoka ghafla kwa matatizo ya kifamilia akiwa tayari amerpanga kikosi cha kwanza katika mechi hiyo ya kirafiki ya juzi, akiwapanga  myota mpya Fernandinho aliyesajiliwa kwa pauni mil 30 na Yaya Toure katika kiungo.

No comments:

Post a Comment