Friday, July 26, 2013

Kocha mpya awahofia Messi, Neymar
Gerardo Martino
KOCHA mpya wa Barcelona, Gerardo Martino ametua rasmi Camp Nou na
kusema utakuwa mtihani mgumu kwake kama Lionel Messi na Neymar hawatang’ara katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo.
Akizungumza kwa mara ya kwanza jana baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili, Gerardo alisema wazi ana kazi kubwa ya kuwamudu nyota hao wawili.
Alisema kutokana na umahiri wao, anajiona mwenye kazi ya ziada ya kuhakikisha nyota hao wawili wanacheza kwa ufanisi katika kikosi cha kwanza.
Lakini, akajifariji kwa kusema Neymar, aliyetua hivi karibuni kwa mkataba wa miaka mitano na Messi, nyota bora wa Dunia mara nne, hawatamwangusha.
"Kama Messi na Neymar watashindwa kucheza pamoja kwa ufanisi, itakuwa ni pigo kwangu kama kocha," alisema na kuongeza kuwa, jukumu kubwa kwake kuhakikisha wanaisaidia timu kushinda.
"Naamini Barca kwa kuwa na wachezaji hawa, itapata mafanikio makubwa. Kazi yangu ni kuwafanya wachezaji wanifahamu na kuniamini ili kuboresha kiwango,” alisema.
Kocha huyo ambaye ni mara ya kwanza kufundisha Ulaya, amepewa juhumu la timu hiyo kuchukua nafasi ya Tito Vilanova aliyepumzikoa kutokana na matatizo ya kiafya. 

No comments:

Post a Comment