Friday, July 19, 2013

Fabregas
Wenger: Man United hawampati Fabregas
KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger amewakatisha tamaa Manchester United kuhusu kumwania Cesc Fabregas wa FC Barcelkwa ya Hispania akisema wanajisumbua bure kwani hawatampata kwa msimu huu.
Wenger aliyewahi kumwania nyota huyo bila mafanikio kumrejesha Emirates msimu ujao ikiwa ni misimu miwili tangu aondoke Emirates, alisema Fabregas hawezi kwenda Old Trafford.
Alisema hiyo inatokana na Fabrega kutamka wazi kuwa bado anapenda kubaki Barcelona, hivyo Manchester United wanajisumbua bure kumwania mchezaji huyo.
Alisema kwa mazingira haoni sababu ya kuongeza dau kwa Fabregas kumzuia kwenda Old Trafford kwani anaamini hawezi kuondoka Camp Nou msimu huu.
Kauli hiyo inatokana na Arsenal kukwama kumrejesha Fabregas kwa dau la pauni mil 29, hivyo hofu yake ni kwenda Man Utd iliyo tayari kumsajili kwa pauni mil 30.     
"Fabregas ameamua kubaki Barcelona," alisema Wenger mbele ya waandishi wa Habari juzi na kuongeza:
Vita ya kumwania Fabregas ni kutokana na shauku ya nyota huyo kukosa uhakika wa namba katika kikosi cha kwanza cha Barcelona tangu arejee akitokea Arsenal miaka miwili iliyopita.
Haya hivyo, kitendo cha kuondoka kwa Thiago aliyetimkia Bayern Munich  ya Ujerumani, kumeongeza uzito wa kubaki kutokana na presha ya namba kupungua katika nafasi ya kiungo chini ya Kocha Tito Vilanova.
Mapema wiki hii, Vilanova alisema nyota huyo mwenye umri wa miaka 26, angependa kubaki Camp Nou kuboresha kiwango chake zaidi.
"Najua amepata ofa nyingi. Lakini nimezungumza naye amenieleza angependa kubaki.
"Hana mpango wa kwenda kwingine. Anajua kuwa hapa ndipo mahali anapoweza kucheza michuano ya kimataifa. Ndoto yake ni kupata mafanikio hapa."

No comments:

Post a Comment