Friday, July 26, 2013

CASTLE LAGER yaileta Barcelona Afrika
Makamu wa Rais wa Barcelona, Josep Maria Bartomeu akimkabidhi Mkurugenzi wa Masoko Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Kashililla Thomas, amletee Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete. TBL kupitia bia yake ya Castle jana iliingia mkataba wa ushirikiano wa miaka mitatu na klabu hiyo kwa upande wa Afrika.
BIA ya Castle Lager, jana iliingia makubaliano ya kuidhamini klabu maarufu Duniani, FC Barcelona ya Hispania kwa kipindi cha miaka mitatu udhamini utakaokifanya kinywaji
hicho kuwa bia rasmi ya klabu hiyo Afrika.
Hafla ya ushirikiano huo iliyofanyika kwenye uwanja wa Camp Nou, unaifanya CASTLE Lager kuwa bia rasmi itakayotumika kwa shughuli yoyote ambayo Barcelona itashiriki Afrika.
Aidha, chini ya ushirikiano huo, FC Barcelona itafungua milango kwa mashabiki wake Barcelona Afrika kuwa karibu na wachezaji wa Barcelona, vifaa na kumbukumbu.
Aidha, itapata nafasi ya kusafiri kwenda Hispania kushuhudia kwa karibu timu ya Barcelona.
Mkataba huu utakuwa maalum kwa ajili ya CASTLE Lager kwenye nchi nyingi za Afrika isipokuwa kwa baadhi ya nchi chache zilizochaguliwa ambapo itatumika Castle Milk Stout.
Ni mara ya kwanza kwa timu ya FC Barcelona kusaini mkataba
wa udhamini na kampuni ya bara la Afrika. Kushirikiana na bia bingwa Afrika litaongeza kwa haraka umaarufu wa timu ya FC Barcelona ndani ya bara la Afrika na kufungua milango kwa mashabiki wa klabu hii kupata bidhaa mbalimbali za Barcelona na nafasi za kushinda safari ya kwenda Barcelona kuitembelea klabu hiyo.
“Tumefurahi sana kuingia katika ushirikiano na Castle Lager na Castle Milk Stout, chapa zinayofahamika dunia nzima. Tunafanana na Castle kwa kuwa sote tuna historia ya zaidi ya miaka 100 na utamaduni uliotukuka. Na sote tuna mapenzi na mpira wa miguu pamoja na mashabiki wake katika soko muhimu kama Afrika,” alisema Javier Faus, Makamu wa Rais wa FC Barcelona anayeshughulikia masuala ya uchumi.
“Uamuzi wa Barcelona kuingia ushirika na na bia inayoongoza barani Afrika kutaongeza umaarufu wa bia hiyo kwenye bara hili na kuwawezesha wachezaji wa timu hiyo kufika maeneo amabyo hawajawahi kufika barani Afrika,” alisema David  Carruthers Mkurugenzi wa Masoko wa SabMiller Afrika (kampuni mama ya TBL).
CASTLE Lager si bidhaa mpya kwenye udhamini wa mpira wa miguu na vyama, ina miaka mingi ya kujihusisha katika soka barani Afrika kwa kipindi cha miaka 85 kupitia ligi mbalimbali za nchi tofauti kama vile Zimbabwe, Swaziland, Botswana, Lesotho na pia mashindano ya kanda kama COSAFA Kusini mwa Afrika na CECAFA Afrika Mashariki.
Kutokana na soka la Ulaya kupata umaarufu mkubwa na mashabiki wengi barani Afrika, Castle Lager imekuwa ikidhamini urushaji wa matangazo ya ligi hizo kwenye televisheni barani Afrikana kuwapa mashabiki fursa ya kufatilia kila kinachoendelea kwenye ligi hizo maarufu duniani ambazo ni Ligi Kuu ya Ulaya, Ligi Kuu ya Uingereza na La Liga ya Kihispania.
Kufuatia udhamini huu, wanywaji wa Castle Lager na Castle Milk Stout pamoja na mashabiki wa Barcelona barani Afrika sasa watarajie mambo mengi ya kusisimua katika ulimwengu wa soka. 

No comments:

Post a Comment