Wednesday, July 31, 2013

Azam Tv yawachanganya Yanga
SAKATA la Klabu ya Yanga kugomea udhamini wa Azam Tv katika Ligi Kuu Tanzania bara, limezidi kupata nguvu baada ya viongozi wa matawi ya klabu hiyo kubariki msimamo huo wa uongozi.
Msimamo huo ulitolewa jana na viongozi wa matawi ya klabu hiyo jijini Dar es Salaam ambao walikutana kujadili suala hilo na kusema wanaunga mkono.
Akizungumza kwa niaba ya wenzake, Bakili Makele alisema viongozi wao (Yanga) wapo sahihi kujitoa kwenye udhamini huo na kusema wanapata shaka na uharaka ya Kamati ya Ligi katika suala hilo.
Bakili alisema licha ya kutowekwa kwa tenda ya suala hili ili kushindaniwa katika mazingira ya wazi, pia jambo hilo lingeachwa lishughulikiwe baada ya uchaguzi Mkuu wa Shirikisho la soka la Tanzania (TFF).
Kutokana na dosari hizo, wanachama hao wamemsihi Rais wa TFF, Leodegar Chilla Tenga kuingilia kati na kusema wanahofia jambo hilo limeharakishwa kwa maslahi binafsi.
“Jamani tamko letu ni kwamba, tunaungana na viongozi wetu, kwani Yanga ndio kila kitu hapa nchini, Na Azam Tv, inataka kutuchanganya,” alisema Bakili.
Hata hiyo Makele alionekama kutoa kauli zenye mwelekeo wa wivu wa maendeleo kwa kusema kitendo cha Azam Tv kumiliki haki za Ligi Kuu, kutainufaisha klabu ya Azam.
“Jamani, kitendo cha Azam TV kumiliki haki za Ligi Kuu, kutaifanya timu yao izidi kupata kipato, hivyo ving’amuzi vyao tusinunue,” alisema Makele na kuikiwa na viongozi wenzake wa matawi ….Yanga Oyeeeee.
Mwandishi Wetu ilipomtafuta Katibu Mkuu wa klabu hiyo Laurance Mwalusako  ni kwanini walikubali jambo likiwa kwenye mchakato, alisema walijaribu bila mafanikio.
“Ni kweli kwenye vikao tulikuwepo, lakini hatukuafiki kabisa na ndio maana nikasubiri tulifikishe kwa kamati ya utendaji ili wafanye,” alisema Mwalusako.
Kauli hiyo ya Mwalusako imekuja kutokana na wadau kuhoji mantiki ya klabu hiyo kupinga suala hilo wakati Yanga iliwakislishwa na yeye Mwalusako na Makamu Mwenyekiti, Clement Sanga.
“Sisi tuliomba kuona mkataba kwanza, ili tujue haki na mambo katika mkataba huo,  lakini TFF ilikagoma kwa kusema yatosha kusomewa.
Alipotafutwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ligi, Wallace Karia kuhusu msimamo huo wa wanachama, alisema hawana muda kuzozana wanasubiri kufanyia kazi taarifa rasmi itakayofika kwao.
“Yanga ilikuwa na wajumbe wake katika mchakato mzima wa jambo hili, hivyo hatuoni tija kurumbana nao katika kipindi hiki. Kama kweli wamegomea, watuarifu rasmi kwa maandishi.

No comments:

Post a Comment